/*Start Css Menu*/ .menu{ border:none; border:0px; margin:0px; padding:0px; font-family:verdana,geneva,arial,helvetica,sans-serif; font-size:14px; font-weight:bold; color:8e8e8e; } .menu ul{ background:url(http://3.bp.blogspot.com/-jEZvPu90bIA/TjlATeBIGoI/AAAAAAAAE4A/shxxdvs2fHI/s1600/menu-bg.gif) top left repeat-x; height:43px; list-style:none; margin:0; padding:0; } .menu li{ float:left; padding:0px 8px 0px 8px; } .menu li a{ color:#666666; display:block; font-weight:bold; line-height:43px; padding:0px 25px; text-align:center; text-decoration:none; } .menu li a:hover{ color:#000000; text-decoration:none; } .menu li ul{ background:#e0e0e0; border-left:2px solid #a80329; border-right:2px solid #a80329; border-bottom:2px solid #a80329; display:none; height:auto; filter:alpha(opacity=95); opacity:0.95; position:absolute; width:225px; z-index:200; /*top:1em; /*left:0;*/ } .menu li:hover ul{ display:block; } .menu li li { display:block; float:none; padding:0px; width:225px; } .menu li ul a{ display:block; font-size:12px; font-style:normal; padding:0px 10px 0px 15px; text-align:left; } .menu li ul a:hover{ background:#949494; color:#000000; opacity:1.0; filter:alpha(opacity=100); } .menu p{ clear:left; } .menu #current{ background:url(http://1.bp.blogspot.com/-NjNjSmAlq34/TjlATMvGF7I/AAAAAAAAE38/UxPs9Qg4Fyg/s1600/current-bg.gif) top left repeat-x; color:#ffffff; } /*End Css Menu from http://www.spiceupyourblog.com*/

Powered by Blogger.

Habari

       WAASI WALAANIWA KWA MAUAJI SYRIA!!

Wapiganaji wa kundi la waasi nchini Syria wamelaaniwa vikali baada ya picha moja ya video iliyowekwa kwenye mtandao wa internet kuwaonyesha wakiwauwa kwa kuwapiga risasi wanaume kadhaa walioshutumiwa kuwa wanamgambo wanaoiunga mkono serikali.
     Waasi wakiwazuilia wanamgambo wanaoiunga mkono serikali
Shirika la kutetea haki za binadamu, Human Rights Watch, picha hiyo, ambapo wanaume hao wanawekwa ukutani na kisha kumiminiwa risasi-huenda inaonyesha vitendo vya uhalifu wa kivita.
Picha za kutisha zimewaonyesha waasi wenye silaha wakiwaua kikatili watu wanaoaminika kuiunga mkono serikali ya Rais assasd katika mji wa Aleppo.
Video hiyo iliyorekodiwa na wanaharakati inaonyesha zaidi ya mateka kumi na wawili waliotambuliwa kama wafuasi wa kundi la wapiganaji la Shabbiha wanaounga mkono serikali.
Wanadaiwa kuwaua wapiganaji kumi na watano wa kundi la waasi la Free Syrian army katika siku za hivi karibuni.
Video hiyo inaonyesha kiongozi wa waasi na wafuasi wake kadhaa wakipelekwa katika eneo na kundi la wapiganaji wenye silaha waliokuwa wakishangilia.
Wanapelekwa hadi karibu na ukuta na kisha wanapigwa risasi na miili yao kuwekwa pamoja. Kumekuwepo ripoti za wapiganaji kutekeleza vitendo vya unyanyasaji lakini vitendo hivyo havijawahi kurekodiwa.
Ni wazi kuwa waasi wanadhibiti maeneo kadhaa ya mji wa Aleppo na kuendelea katika maeneo mengine. Kuna ripoti kuwa huenda wamepata msaada wa silaha zenye uwezo wa kudhibiti mashambulio ya serikali.
Wanaharakati wanasema majeshi ya serikali yamewaua watu wengi katika mapigano ya hivi karibuni katika vitongoji vya mji mkuu Damascus.
Baraza la kitaifa la upinzani nchini Syria limeshtumu waasi hao wenye silaha kwa kuwaua wafungwa wanao unga mkono sererikali katika mji wa Aleppo. Shirika la kutetea haki za binadam la human rights watch limesema video hiyo inaonyesha vitendo vya uhalifu wa kivita.


ZITTO KABWE AIBULIWA NA KASHFA YA RUSHWA!!

Katika gazeti la Mwananchi la tarehe 23 Julai 2012, kulikuwa na habari yenye kusomeka ‘Wabunge wamsafishia Zitto njia ya Urais 2015′. Habari hii imeleta mjadala mara baada ya kutoka na kusomwa. Mjadala umekuzwa zaidi baada ya Wabunge ndugu Halima Mdee na ndugu Joshua Nassari kukanusha maneno waliyonukuliwa kuyasema. Napenda kusema masuala yafuatayo.
Moja, Waheshimiwa Wabunge Halima Mdee, Joshua Nassari, Kangi Lugola, Esther Bulaya, Deo Filikunjombe, Raya Ibrahim, Amina Mwidau na David Kafulila walihudhuria tamasha la vijana wa Kigoma All Stars kwa kualikwa na Mratibu wa kundi hilo Mwasiti Almasi.
Wabunge wengine walialikwa lakini hawakutokea wakiwemo Joseph Mbilinyi, David Silinde, Amos Makala, Vicky Kamata na Peter Serukamba. Wabunge hawa hawakualikwa na mimi bali nilisaidia ‘logistics’ tu. Lengo la kushauriana na Vijana wa Kigoma All Stars kuwaalika wabunge kutoka vyama mbalimbali lilikuwa ni kuonyesha umoja na mshikamano wa nchi bila kujali vyama vya siasa.
Wabunge wote walioalikwa waliambiwa hii ni shughuli ya muziki na wala sikufanya mazungumzo nao yeyote ya awali au kuwaambia au kukubaliana nini cha kuzungumza au hapana. Tamasha lilikuwa la muziki na halikuhusika kabisa na siasa. Ni bahati mbaya sana kuwa kuna matamshi ya kisiasa yalitamkwa katika shughuli ile.
Waheshimiwa wote walipewa nafasi ya kusalimia na wote walizungumza. Wabunge waliozungumza kwa muda mrefu kidogo ni ndugu Halima Mdee, Joshua Nassari, Deo Filikunjombe na Kangi Lugola.
Hotuba za Wabunge wote zilirekodiwa kwenye video neno kwa neno na video hizo zitawekwa wazi kwenye blogu yangu kama sehemu ya documentary ya tamasha lile la kihistoria.
Pili, sikuhusika kwa namna yeyote ile na kuandikwa kwa habari hii iliyozusha mjadala. Wala sikujua kama habari hii ingeandikwa maana katika ziara ile sikuita mwandishi hata mmoja maana nilitaka liwe tukio la Kigoma tu. Mimi kama mlezi wa KigomaAllStars na vijana wenyewe tulijikita katika ‘shukrani Kigoma’ kwa watu wa Kigoma.
Kama mwandishi kaandika ambayo wabunge hawa hawakuyasema basi itaonekana kwenye videos hizo. Wabunge wenyewe wanajua kwenye nafsi zao nini walisema Kigoma na kipi kiliwasukuma kusema walioyasema Kigoma.
Nisingependa kuhusishwa kwa njia yeyote ile na matamshi yao, habari iliyowanukuu na hata makanusho yao. Maana mwisho wa siku ukweli ndio utasimama.
Suala la Urais lisitupotezee muda kwani kuna mambo mengi sana ya kujadili kuhusu nchi yetu. Taharuki ambazo watu wanazipata masuala ya urais yanapotajwa zinashangaza sana.
Chama changu bado hakijatangaza rasmi mchakato wa kupata mgombea Urais. Hivi sasa chama hakina mgombea Urais mpaka hapo mchakato utakapotangazwa ambapo wanachama wataruhusiwa kuomba kupeperusha bendera ya chama. Mwanachama wa chama chetu atakaye kubalika na jamii na wajumbe wa mkutano wa uteuzi ndiye atakuwa mgombea wetu. Kwa sasa hayupo na hivyo tusipoteze muda kujadili jambo hili.
Mzee Thabiti Kombo alituachia usia tunapokuwa tunazungumza. Alisema ‘weka akiba’ sio akiba ya fedha, bali ya akiba ya maneno. Tuweke akiba ya maneno. Tusimalize yote.



MISAADA ZAIDI  YASITISHWA NCHINI RWANDA
Serikali ya Uholanzi imesitisha msaada wa dola milioni 6.15 kwa Rwanda baada ya nchi hiyo kuhusishwa na ufadhili wa waasi katika Jamuhuri ya kjidemokrasia ya Congo.
Hatua hii inajiri siku kadhaa baada ya Marekani kutangza inanuia kupunguza msaada wa kijeshi kwa Rwanda.
Hata hivyo Rwanda imekuwa ikikanusha madai ya umoja wa mataifa kuwa inafadhili kundi la waasi wa M23 mashariki mwa DR Congo.
Waasi hao walianza kutoka jeshini kuanzia mwezi Aprili na hadi kufikia sasa takriban watu 200,000 wametoroka makwao kwa sababu ya mapigano kati ya jeshi na waasi hao.
Hatua hii ya Udachi inajiri baada ya afisaa mkuu wa umoja wa mataifa kuambia BBC kuwa wanajeshi wanaotoka katika jeshi la DRC wamekiri kusajiliwa na Rwanda.
Mnamo siku ya Alhamisi, Umoja wa mataifa uliripoti kuwa wana
jeshi wake walisaidia jeshi la DRC kuwafukuza waasi hao kutoka mji wa Goma kwa kutumia helikopta pamoja na magari ya kijeshi.

Mfumo wa sheria.

Mwandishi wa BBC mjii Hague, Anna Holigan, anasema kuwa hii ndio hatia ya kwanza ya kifedha kuwa rais Kagame huenda ameanza kuwapoteza washirika wake wa Ulaya.
Waziri wa mambo ya nje wa Uholanzi, amethibitisha kuwa kuanzia sasa haitafadhili vyovyote serikali ya Rwanda hadi pale itakapoweza kuhakikishiwa na Rwanda kuhusiana na madai hayo.
Pesa hizo ilizokuwa inapokea Rwanda zilikuwa zinatumika kuinia hadhi ya mfumo wa sheria wa Rwanda, ingawa mashirika yasiyo ya kiserikali yataendelea kufadhiliwa.

Serikali ya Udachi hata hivyo ingali inasubiri jibu kutoka kwa Rwanda kuhusiana na hatua hiyo wakati ikiendelea kushauriana na nchi zingine za Ulaya kuhusu hatua zaidi dhidi ya Rwanda.

0 comments:

Post a Comment